Music, Comedy, HD, TV Shows, Movies

Wednesday, July 8, 2015

MO, DIAMOND PLATNUMZ KUTIKISA SINGIDA MJINI MCHANA HUU

No comments :
IMG_7330

Mbunge wa Singida mjini, Mh. Mohammed Dewji akishuka kwenye ndege mara tu baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Singida.



IMG_7331



Mh. Mohammed Dewji akilakiwa na Mjumbe wa halmashauri kuu CCM (NEC) taifa manispaa ya Singida, Hassan Mazala mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Singida mjini kwa ajili kuhutubia Mkutano mkubwa ambao atawasilisha taarifa ya utekelezaji wa ilani ya mwaka 2005/2010 na 2010/2015 ambapo Mwanamuziki wa kimataifa Nassib Abdul almaarufu kama Diamond Platnumz atatumbuiza wanaSingida. Kushoto ni Mwenyekiti wa CCM wilaya Singida, Jumanne Hamis Nguli.



IMG_7333



Mh. Mohammed Dewji akisalimiana na Katibu wa CCM wilaya ya Singida mjini, Magdalena Ndweta.



IMG_7334



Mh. Mohammed Dewji akisalimiana na Katibu ambaye pia ni Mjumbe wa kamati ya siasa ya wilaya Singida mjini, Duda Juma.



IMG_7336



Mwanamuziki wa kimataifa nchini, Diamond Platnumz akilakiwa na Mwenyekiti wa CCM wilaya Singida, Jumanne Hamis Nguli.



IMG_7341



Mh. Mohammed Dewji akionekana mwenye furaha na tabasamu bashasha akiongoza na Mwenyekiti wa CCM wilaya Singida, Jumanne Hamis Nguli kusalimiana watoto na wananchi waliojitokeza kumlaki katika uwanja wa ndege wa Singida mjini.



IMG_7343



Umati wa watoto wanaoishi karibu na maeneo ya uwanja wa ndege wa Singida mjini wakiwa wamefurika kwenye uwanja huo kumpokea mbunge wao.



IMG_7344



Pichani juu na chini watoto na vijana wakimfurahia Mbunge wao Mh. Mohammed Dewji.



IMG_7345



IMG_7347



IMG_7351



Diamond Platnumz akigombaniwa na wakazi wa Singida mara tu baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Singida.



IMG_7352



Mwanamuziki wa kimataifa Diamond Platnumz, Rommy Jones pamoja na mlinzi wake wakielekea kwenye gari maalum mara tu baada ya kuwasili.



IMG_7353



Wananchi wa Singida mjini wakimsindikiza Mbunge wao Mh. Mohammed Dewji.



IMG_7356



IMG_7357



CCM Oyeeeeeeee!!!



 

No comments :

Post a Comment